Soma, ewe Nabii, Qur’ani uliyoteremshiwa ukianza kwa Jina la Mola wako Aliyepwekeka kwa kuumba
Aliyemuumba kila binadamu kwa pande la damu nzito nyekundu
Soma, ewe Nabii, kile ulichoteremshiwa, na Mola wako ni Mwingi wa wema, Mwingi wa ukarimu
Aliyewafundisha viumbe vyake kuandika kwa kalamu
Alimfundisha binadamu vitu ambavyo hakuwa akivijua. Akamtoa kwenye giza la ujinga, Akampeleka kwenye nuru ya elimu
Kweli, binadamu hukiuka mipaka ya Mwenyezi Mungu
akijiona ametosheka kwa utajiri wake
Basi, ajue kila mwenye kutupa mipaka kuwa mwisho atarudi kwa Mwenyezi Mungu Ambaye Atamlipa kila binadamu kwa alilolitenda
Je, umeona ujeuri wa ajabu zaidi kuliko wa mtu huyu, Abu jahl
Anayemkataza mja wetu, Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, anapomsalia Mola wake
Waonaje iwapo mwenye kukatazwa kusali yuko uongofuni, vipi anamkataza
Au iwapo anaamrisha mwigine kumcha Mungu, vipi anamkataza hilo
Waonaje iwapo huyu mwenye kukataza anakanusha lile alinganiwalo kwalo na kulipa mgongo
hajui kuwa Mwenyezi Mungu anaona kila analolifanya
Basi mambo si kama anvyodai Abu Jahl. Na asipokomeka na ushindani alionao na udhia wake, Tutamshika upaa wake kwa nguvu na kumtia Motoni
Upaa wake ni upaa wenye maneno ya urongo na vitendo vya makosa
Basi na awalete, mtupaji mipaka huyu, watu wa baraza ili wamsaidiye
Sisi Tutawaita Malaika wa adhabu
Mambo si kama Abu Jahl anavyoyadhania. Yeye, ewe Mtume, hawezi kukufanya lolote la kukudhuru Usimfuate kwa lile alilokuitia la kuwa uache Swala, bali msujudie Mola wako na uwe karibu na Yeye kwa kujipendekeza Kwake kwa kumtii